Joyciline Jepkosgei ashinda Barcelona Half Marathon

Dismas Otuke
1 Min Read

Mshikilizi wa zamani wa rekodi ya dunia ya nusu marathon Joyceline Jepkosgei, ameibuka mshindi wa makala ya mwaka huu ya mbio za nusu marathoni za Barcelona zilizoandaliwa Jumapili nchini Uhispania./strong>

Jepkosgei, ambaye ni bingwa wa London mwaka 2021, ameziparakasa mbio hizo kwa kutumia muda wa saa 1 dakika 4 na sekunde 13.

Alexandra García Jadraque wa Uhispania alimaliza wa pili kwa saa 1 dakika 5 na sekunde 28, huku Gladys Chepkurui wa Kenya akinyakua nishani ya shaba kwa saa 1 dakika 6 na sekunde 25.

Mbio za wanaume zilishindwa na Mganda Jacob Kiplimo.

Website |  + posts
Share This Article