Idara ya uhamiaji yapiga jeki mpango wa Usajili Mashinani

Dismas Otuke
1 Min Read

Idara  ya Uhamiaji imeendeleza zoezi la usajili wa Wakenya kuchukua vitambulisho vya kitaifa  maarufu kama Usajili Mashinani.

Maafisa wa idara hiyo walizuru  taarafa ya Laisamis kaunti ya  Marsabit  mwishoni mwa juma na kuwasaidia wasio na vitambulisho kujisajili bila malipo.

Hatua hiyo ya serikali inalenga kuwapunguzia wananchi mzigo wa kusafiri kwa mwendo mrefu hadi vituo vya kujisajili ili kupata kitambulisho cha kitaifa.

Ni wiki ya pili  tangu serikali ianzishe zoezi hilo.

Zoezi sawi liliandaliwa katika kaunti za Samburu na Isiolo katika juhudi za kuleta huduma karibu na wananchi.

 

 

Share This Article