Timu ya taifa Harambee Stars imeimarisha mazoezi leo Jumatatu katika uwanja wa Police Sacco kujiandaa kwa mechi ya kufuzu kwa Kombe la Dunia mwaka 2026 dhidi ya Burundi.
Kenya itachuana na Burundi Alhamisi hii katika mchuano wa kufuzu kwa Kombe la Dunia.
Baadaye Kenya chini ya ukufunzi wa kocha Benni McCarthy itasafiri kuelekea mjini Abidjan kuchuana na Ivory Coast Jumanne ijayo.