FIFA yazindua Trionda, mpira wa Kombe la Dunia mwaka 2026

Dismas Otuke
1 Min Read
ZURICH, SWITZERLAND - OCTOBER 02: FIFA World Cup 2026 Official Match Ball at the Home of FIFA on October 02, 2025 in Zurich, Switzerland. (Photo by Marcio Machado/FIFA)

Shirikisho la Soka Duniani FIFA limezindua mpira rasmi wa Trionda utakaotumika katika mechi za fainali za Kombe la Dunia mwaka ujao kwa pamoja na mataifa ya Canada, Mexico na Marekani.

Hafla hii imeandaliwa mapema leo Ijumaa zikiwa zimesalia siku 250, kabla ya kungóa nanga kwa kindumbwendumbwe hicho kitakachoshirikisha mataifa 48 kwa mara ya kwanza.

Mpira huo una rangi tatu za kijani, nyekundu na samawati zinazoashiria mataifa matatu yatakayoandaa kipute hicho.

 Rais wa FIFA Gianni Infantino akizindua mpira rasmi wa Kombe la Dunia

Droo ya Makala ya 23 ya Kombe la Dunia imeratibiwa kuaandaliwa mjini Washington, Marekani, Disemba 5 mwaka huu.

Website |  + posts
Share This Article