Comoros imetangaza kusitisha mpango wake wa kuongeza bei ya mafuta siku ya Jumamosi, kufuatia maandano ya kitaifa kupinga ongezeko la bei ya mafuta.
Hii inafuatia kuuawa kwa mtu mmoja na wengine watano kujeruhiwa vibaya wakati wa makabiliano baina ya polisi na waandamanaji hao.
Barabara zilifungwa wakati wa maandamano hayo ya Ijumaa kwa mawe kuendeleza mgomo wa kitaifa ulianza nchini Comoros Jumatatu iliyopita.
Serikali ya Comoros iliongeza bei ya Dizeli kwa asilimia 46 na asilimia 35 kwa bei ya Petroli.
Bei ya mafuta imeongezeka kote duniani kufuatia vita vinavyoendelea eneo la Mashariki ya kati.
Wenye magari ya usafiri wa umma na wenye maduka walisambaratisha usafiri na shughuli za kawaida karibu na mji mkuu wa Moroni.
Mgomo huo na maandamano ulisitishwa Jumamosi baada ya serikali kusema haitaongeza bei ya mafuta ilivyokuwa imetangaza awali.