Baringo kuandaa mashindano ya Rhino Charge mwaka huu

Mashindano hayo ambayo hushirikisha magari ya four wheel yanayoshindana mbugani, yanalenga kuchangisha pesa za kuhifadhi mbuga za wanyamapori na vyanzo vya maji

Dismas Otuke
1 Min Read

Kaunti ya Baringo imetangazwa kuwa mwenyeji wa makala ya 36, ya mashindano ya magari ya Rhino Charge mwaka  huu.

Mashindano hayo ambayo hushirikisha magari ya four wheel yanayoshindana mbugani, yanalenga kuchangisha pesa za kuhifadhi mbuga za wanyamapori na vyanzo vya maji

Tangazo hilo limetolewa leo na karani wa mkondo wa mashindano hayo Don White,katika hafla ya uzinduzi iliyoandaliwa katika shule ya Braeburn kaunti ya Nairobi , na kuhudhuriwa na madereva,wafadhili,maafisa waandalizi,wasimamizi wa kambi na makarani wa mkondo.

Mashindano hayo yanayoandaliwa na shirika la Rhino Ark Charitable Trust, huchangisha mamilioni  ya pesa kila mwaka ambazo huelekezwa kwa kulinda na kuhifadhi vyanzo vya maji ikiwemo Aberdare Range, Mt. Kenya,msitu wa Mau na ule wa Kakamega.

Website |  + posts
Share This Article