Matumaini ya Kenya kutwaa angaa ubingwa mmoja katika makala ya kwanza ya mashindano ya Dunia ya Ultimate mjini Budapest,Hungary yametumbukia nyongo baada ya bingwa wa dunia na Olimpiki Emmanuel Wanyonyi kumaliza wa tatu katika fainali ya mita 800.
Wanyonyi alivuka mstari wa mwisho kwa muda wa dakika 1 sekunde 42.44.
Djamel Sedjaati wa Algeria alitoka nyuma na kutwaa ubingwa kwa dakika 1 sekunde 41.91,mbele ya Marco Arop wa Canada aliyemaliza wa pili.
Awali, Julius Yego alimaliza wa sita katika urushaji sagai alirusha umbali wa mita 80.23, huku Rumesh Pathrage wa Srilanka akishinda kwa kurusha mita 91.09.
Timothy Cheruiyot na Phanuel Kosgei wamemaliza katika nafasi za nane na kumi katika mita 1500,mbio zilizoshindwa na Josh Kerr.