Wenyeji Kenya watachuana na Cameroon katika nusu fainali ya Kombe la Afrika Alhamisi hii huku wakilenga kutetea kombe hilo.
Malkia Strikers walifuzu kwa nusu fainali kufuatia ushindi wa seti 3-1 dhidi ya Algeria Jumanne usiku katika ukumbi wa Kasarani.
Kenya ilipoteza seti ya kwanza 21-25, kabla ya kutwaa seti zilizofuatia 25-7,25-15 na 25-18, na kujikatia tiketi kwa nusu fainali.
Cameroon walifuzu kwa nusu fainali kufuatia ushindi wa seti 3-0 dhidi ya Uganda.
Nusu fainali ya kwanza itakuwa kati ya Misri na Rwanda kuanzia saa kumi baada ya Rwanda kuwatema Ghana seti 3-1 huku Misri ikiwabandua Tunisia seti 3-0.
Fainali ya mashindano hayo ni Jumamosi hii huku washindi wakifuzu kwa mashindano ya Dunia mwaka ujao na pia Michezo ya Olimpiki ya mwaka 2028.