Serikali ya Nepal imeonya kuhusu uwezekano wa kuzuka kwa mafuriko zaidi ,ikiwataka wakazi walio karibu na maeneo yaliyokumbwa na mafuriko ya wiki jana kuhama huku viwango vya maji katika mto wa Bhotekoshi vikipanda.
Serikali ilituma jumbe kwa rununu za raia wake mapema Jumapili kuwatahadhari kutokea kwa mafuriko zaidi katika maeneo mengine ikiwemo barabara kuu ya Kathmandu, iliyoathiriwa katika mafuriko ya wiki jana.
Vifo vilivyotokana na mafuriko ya wiki jana nchini Nepal, na eneo la Tibet nchini Uchina, vimepanda na kufikia 800, huku zaidi ya watu 3,000 wakiwa hawajulikani waliko.

Nepal imetangaza jumla ya vifo 734 huku watu 2nd 498 wakiwa hawajulikani waliko,ilihali serikali ya Uchina imeripoti vifo 16 na watu wengine of 546 wakitoweka.
Watu wapatao 93,000 nchini Nepal, wameathiriwa na mkasa huo mbaya zaidi kuwahi kutokea kulingana na shirika la msalaba Mwekundu.