Jeshi la Uganda, UPDF litaandaa mashindano ya mwigo wa kivita katika uwanja wa Uhuru wa Kololo viungani mwa mji wa Kampala.
Zoezi hilo litakaloshirikisha wanajeshi zaidi ya 1400 kutoka timu 40 za vikosi vyote vya jeshi litaandaliwa kati ya Agosti 22 na 25.
Timu 5 bora pia zitashiriki mashindano ya mtindo huria ambao unajumuisha ubunifu, uweledi na tamaduni za Kiganda.
Fainali ya mashindano hayo itahudhuriwa na mshauri wa Rais wa masuala ya kijeshi Jenerali Kainerugaba Muhoozi Agosti 25.