Katibu katika Wizara ya Fedha Dkt. Chris Kiptoo leo Jumatatu amewaongoza Wakurugenzi Wakuu na Wakuu wa Idara kupigia msasa hatua zilizopigwa katika kutekeleza mageuzi muhimu na mipango ya kimkakati katika wizara hiyo.
Wakati wa mkutano huo wa kimkakati wa siku moja, kila kurugenzi inaelezea hatua iliyopiga chini ya madaraka yake, changamoto ilizokumbana nazo, vipaumbele na nyanja zinazohitaji ushirikiano thabiti.
Mazungumzo yakiangazia namna ya kuzikabili changamoto ibuka, kuimarisha uwajibikaji na kuboresha shabaha ya wizara hiyo katika kutoa huduma bora.
“Lengo la mkutano ni kuimarisha utekelezaji, kuharakisha matokeo na kutoa athari kubwa,” alisema Dkt. Kiptoo