Mwimbaji wa Tanzania Zuchu na Diamond Platnumz waliondoka hospitalini jana wakiwa katika msafara mkubwa uliokuwa na zaidi ya magari 50 ya kifahari, yakiwemo Rolls-Royce, baada ya kumpokea mtoto wao wa kwanza wa kike.
Wawili hao walikwenda moja kwa moja hadi nyumbani ambapo mama yake Diamond, maarufu kama Mama Dangote aliwapokea, ili kumtambulisha mtoto huyo mchanga.
Video zilizosambaa mitandaoni zinaonyesha wazazi hao wawili wakitoka kwenye chumba cha hospitali wakiwa wamembeba mwanao na kuabiri mojawapo ya magari ya kifahari yaliyokuwa nje.
Nyingine iliwaonyesha wakifika mlangoni kwa Bi. Sanura ambaye anaacha alichokuwa akifanya na kuwapokea Zuchu akisikika akimwamkua “Shikamoo Mama”, huku mama huyo akimbeba mjukuu wake na kuingia naye sebuleni.
Anapojitahidi kumwondoa mtoto kutoka kwenye kitanda chake, Zuchu anamtania akimwambia “Nimekuletea mke mwenzio,”.
Zuchu alijifungua Agosti 1, 2026 katika hospitali iitwayo Saifee jijini Dar es Salaam, nchini Tanzania, ambapo alipokea wageni wengi tu waliofika na zawadi kumpongeza.