Ivory Coast, Ecuador, Uswidi na Australia zafuzu raundi ya 32 Kombe la Dunia

Kundini F mapema Ijumaa,Uswidi imetoka sare ya bao moja na Japan, na kufuzu kwa raundi ya 32 bora nao Uholanzi wakaongoza kundi hilo baada ya kuwalemea Tunisia mabao 3-1.

Dismas Otuke
1 Min Read

Wawakilishi wa Afrika, Ivory Coast walihitaji mabao mawili ya Nicholas Pepe moja katika kila kipindi ili kufuzu kwa awamu ya 32 waposajili ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya limbukeni Curao, Alhamisi usiku.

Ushindi huo uliwaweka tembo wa Ivory Coast katika nafasi ya pili kwa pointi sita sawia na viongozi Ujerumani, licha ya kuambulia kichapo cha 2-1 kutoka Ecuador katika mechi nyingine ya mwisho kundini E.

Kundini F mapema Ijumaa, Uswidi imetoka sare ya bao moja na Japani na kufuzu kwa raundi ya 32 bora, nao Uholanzi wakaongoza kundi hilo baada ya kuwalemea Tunisia mabao 3-1.

Katika kundi D, Marekani ambayo tayari ilikuwa imejihakikishia nafasi ya kwanza ilipigwa magoli 3-2 nyumbani na Uturuki ambao tayari wameyaaga mashindano huku Paraguay na Australia zikitoka sare tasa, matokeo yaliyozivusha timu zote kwa raundi ya 32 bora.

Share This Article