FIFA World Cup 2026: Mkenya Ouko kusimamia mechi uwanjani Mercedes Benz

Uga huo aidha utaandaa mechi moja ya raundi ya 32, moja ya raundi ya 16 na nusu fainali moja.

Dismas Otuke
1 Min Read

Difenda wa zamani wa timu ya taifa Harambee Starlets Terry Ouko, ameteuliwa kusimamia mechi zitakazochezwa katika uwanja wa Mercedes-Benz mjini Atlanta nchini Marekani.

Ouko atasimamia na kuhakikisha viwango vya FIFA kuhusu haki za kibinadamu, kukabiliana na ubaguzi na utunzaji mazingira katika mechi tano za makundi na tatu za mwondoano zitakazochezwa katika uwanja huo.

Ouko kwa sasa anahudumu kama Naibu Rais wa chama cha maslahi ya wachezaji (KEFWA), kando na kuketi katika bodi ya kimataifa ya FIFA (FIFPRO).

Mechi za makundi zitakazochezwa uwanjani Mercede Benz nchini Marekani

Juni 15: Spain vs Cape Verde

Juni 18: South Africa vs Czechia

Juni 21: Spain vs Saudi Arabia

Juni 24: Morocco vs Haiti

Juni 27: Uzbekistan vs DR Congo

Uga huo aidha utaandaa mechi moja ya raundi ya 32, moja ya raundi ya 16 na nusu fainali moja.

Share This Article