World Cup 2026: Fahamu viwanja vitakavyoandaa mechi za Kombe la Dunia nchini Mexico

Zimesalia siku 9 kabla ya kuanza kwa Kombe la Dunia

Dismas Otuke
2 Min Read

Mexico itaandaa jumla ya mechi 13 za Kombe la Dunia katika miji ya Guadalajara, Monterrey na Mexico City baina ya Juni 11 na Julai 19 mwaka huu.

Uwanja wa Guadalajara

Uwanja huu ulifunguliwa mwaka 2010, kabla ya kukarabatiwa kwa fainali za mwaka huu za Kombe la Dunia.

Idadi ya mashabiki ambao uwanja huu unamudi ni 48,000.

Mechi za Kombe la Dunia zitakazochezwa uwanjani

South Korea v Czechia, 11 June

Mexico v South Korea, 18 June

Colombia v Democratic Republic of Congo, 23 June

Uruguay v Spain, 26 June

Uwanja wa Mexico City(Azteca)

Uwanja huu unapatikana katika mji mkuu wa Mexico City, na ulijengwa mwaka 1966 kabla ya kukarabatiwa mwaka huu.

Idadi ya mashababiki wanaotoshea katika kiwara hiki ni 83,000.

Mechi za Kombe la Dunia zitakazochezwa katika wa Uwanja wa Mexico City (Azteca)

Mexico v South Africa, 11 June

Uzbekistan v Colombia, 17 June

Czechia v Mexico, 24 June

Round of 32, 30 June (1A v 3CEFHI)

Round of 16, 5 June (W79 v W80)

Uwanja wa  Monterrey

Uwanja huu unafahamika kwa jina la Estadio BBVA na upo mjini Guadalupe, Nuevo León, Mexico

Ni uwanja uliofunguliwa rasmi mwaka 2015  na unamudu mashabiki 53,500

Mechi nne za Kombe la Dunia mwaka huu zitapigwa hapa zikiwa;

Sweden v Tunisia, 14 June

Tunisia v Japan, 21 June

South Africa v South Korea, 24 June

Round of 32, 29 June (1F v 2C)

Zimesalia siku 9 kabla ya kuanza kwa Kombe la Dunia.

 

Share This Article