Ghana yapiga marufuku mapenzi ya jinsia moja

KBC Digital News
2 Min Read

Mapenzi ya jinsia moja nchini Ghana ni marufuku, baada ya Bunge la Taifa hilo la Afrika Magharibi, kuidhinisha mswada mpya unaoharamisha mapenzi ya jinsia moja na uendelezaji wa shughuli za LGBTQ+.

Kulingana na mswada huo, kujitambulisha kama mpenzi wa jinsia moja, mtu aliyebadili jinsia au mpenzi wa jinsia zote mbili kunaweza kuadhibiwa kwa kifungo cha hadi miaka mitatu jela.

Muswada huo pia unaanzisha “wajibu wa kuripoti” vitendo vilivyopigwa marufuku kwa polisi.

Viongozi wa kidini wamemshinikiza Rais John Dramani Mahama, ambaye bado anahitaji kuidhinisha sheria hiyo, kuimarisha sheria zinazopinga mapenzi ya jinsia moja tangu alipoingia madarakani mwaka jana.

Marufuku hiyo imekosolewa vikali na mashirika ya kimataifa, ikiwa ni pamoja na Human Rights Watch, ambayo ilisema inaweka maisha ya watu wa LGBTQ+ hatarini huku pia “ikiwahimiza raia kufuatiliana na kusemana”.

Mahusiano ya jinsia moja yamepigwa marufuku nchini Ghana chini ya sheria zilizoanzia enzi ya ukoloni wa Uingereza.

Katika hotuba yake kwa Bunge, aliyeleta muswada huo Mchungaji John Ntim Fordjour alisema unalinda familia na maadili ya kitamaduni ya Ghana.

Aliongeza kuwa marufuku hiyo mpya itafanya sheria zilizopo kuwa “imara zaidi, zenye kujumuisha mengi zaidi, na masharti magumu zaidi katika kukabiliana na desturi za LGBTQ+”.

Mtu yeyote anayejitambulisha kama “mshirika”, wa neno la jumla linalomaanisha mfuasi wa watu wa LGBTQ+, anaweza pia kukabiliwa na kifungo jela.

Taarifa ya BBC.

TAGGED:
Share This Article