Botswana wapewa mapumziko ya nusu siku baada ya kushinda dhahabu

Dismas Otuke
1 Min Read
GABORONE, BOTSWANA - May 2: at the World Athletics Relays Gaborone 26 on May 2, 2026 in Gaborone, Botswana. (Photo by Christel Saneh for World Athletics)

Wafanyakazi wa umma nchini Botswana, walipewa mapumziko ya nusu siku Jumatatu kusherehekea ushindi wa timu ya mita 400 kwa wanariadha wanne wanaume kupokezana kijiti siku ya Jumapili.

Timu hiyo iliyomjumuisha bingwa wa Olimpiki Letsile Tebogo, ilishinda dhahabu na kuweka rekodi mya ya dakika 2 sekunde 54.47 .

Wafanyakazi wa umma nchini Botswana, walifunga kazi saa sita na dakika 45 Adhuhuri, ili kujumuika na wenzao kwa shamrashamra hizo za ushindi.

Mapumziko hayo yalitangazwa na Mkurugenzi wa huduma za serikali punde baada ya kumalizika kwa mbio za Dunia za kupokezana kijiti  Jumapili jioni mjini Gaborone,Botswana.

Share This Article