Jeshi la Israel limetangaza kuwa limeanza kushambulia miundombinu ya kundi la Hezbollah katika mji mkuu wa Lebanon, Beirut.
Picha zilizopigwa asubuhi zinaonyesha moshi ukifuka kutoka katika vitongoji vya kusini mwa mji huo.
Jeshi la Ulinzi la Israel, (IDF) limesema kuwa linalenga “miundombinu ya kigaidi” ya kundi hilo linaloungwa mkono na Iran.
Vyombo vya habari vya Lebanon pia vimeripoti wimbi jipya la mashambulizi ya anga ya Israel katika eneo la kusini mwa Beirut.
Zaidi ya watu milioni moja wamelazimika kuhama makazi yao nchini Lebanon, huku vita vinavyoihusisha Marekani na Israel dhidi ya Iran vikiendelea kuathiri eneo pana la mashariki ya kati.
Mtoto mmoja aliyezungumza na BBC alisema anahisi “aibu” kulala barabarani baada ya familia yake kulazimika kukimbia makazi yao mjini Beirut.
Taarifa ya BBC