Wanajeshi wenye jinsia bandia kutimuliwa jeshini nchini Marekani yasema serikali ya Rais Donald Trump.
Serikali ya Marekani imetoa arifa kuwa wanajeshi walio na jinsia bandia watatengwa na wenzao wa kiume na kike, hatua ambayo imechangia kuwasilishwa kwa kesi mahakamani kupinga agizo hilo la Rais Donald Trump.
Taarifa ya serikali imetoa maagizo zaidi ikisema kuwa wanajeshi wa jinsia hizo bandia watasitishwa kufadhiliwa na kupewa majukumu ya kijeshi.
Trump alishikilia msimamo kuwa lazima wanajeshi wawe wa jinsia ya kiume au kike.
Jeshi la Marekani lina takriban maafisa 15,000 wenye jisinsia bandia.