Simba washikwa na gugumizi Berkane wakitwaa kombe

Dismas Otuke
1 Min Read

Ndoto ya klabu ya Simba kutoka Tanzania bara, kutwaa kombe la shirikisho ilitibuka Jumapili jioni baada ya RS Berkane kunyakua kombe hilo kwa ushindi wa jumla wa mabao 3-1.

Simba walitoka sare ya bao 1 katika marudio ya fainali uwanjani Amaan kisiwani Zanzibar .

Berkane walikuwa wamesajili ushindi wa mabao 2-0, katika duru ya kwanza wiki jana wakiwa nyumbani.

Berkane wametuzwa dola milioni 2, huku Simba wakipokea dola milioni moja za Marekani kwa kumaliza nafasi ya pili.

 

Website |  + posts
Share This Article