Akizungumza leo Alhamisi katika Ikulu ya Nairobi kwenye mkutano na mafundi mbalimbali wa kaunti ya Nairobi, kiongozi wa taifa alifafanua kuwa mpango wa Linda Jamii unawasaidia kina mama wanapokuwa wajawazito, wanapojifungua na hata baada ya kujifungua.
“Tulikuwa na mpango wa Linda Mama, sasa ni Linda Jamii. Kila mama, Serikali ya Kenya itakulipia kwenda clinic hadi wakati na baada ya kujifungua,” President Ruto said.
Alisema serikali imeongeza ufadhili wa huduma za kina mama wajawazito, ili kuimarisha ubora na kupunguza vifo vinavyotokana na ujauzito na maafa ya watoto wanaozaliwa.
“Zamani, bajeti ya mama kujifungua hospitalini ilikuwa shilingi 4,000. Kwa sasa kupitia mpango wa Linda Jamii bajeti hiyo tumeongeza mara tatu kuhakikisha kwamba kila mama anajifungua mahali ambapo kuna usafi, kuna daktari, dawa na tusipoteze wamama ama watoto wakati wa kujifungua,” he said.
Rais alishikilia kuwa mabadiliko hayo ni sehemu ya mpango mpana wa kutimiza utoaji huduma za afya kwa wote kupitia Halmashauri ya Afya ya Jamii, kuhakikisha kila Mkenya anapata huduma za afya bila kujali hali zao za kifedha.