Waandalizi wenza wa fainali za Kombe la Dunia Marekani watashuka katika uchanjaa wa Los Angeles dhidi ya Paraguay, kwa mechi ya kufungua ratiba ya kundi D katika siku ya tatu .
Timu zote mbili hazijawahinyakua kombe hilo na zitalenga kuanza vyema ili kuwa na fursa ya kufuzu kwa raundi ya 32 bora.
Sawia na waandalizi wengine ;Mexico na Canada pia Marekani, itaandaa sherehe za ufunguzi kabla ya mechi dhidi ya Paraguay.
Ni mara ya kwanza kwa Marekani kuandaa Kombe la Dunia tangu mwaka 1994.