Jordaan achaguliwa Rais wa shirikisho la soka Afrika Kusini kwa muhula wa nne

Jordaan alipata kura 157  dhidi ya  82  za mpinzani wa  karibu Sandile Zungu.

Dismas Otuke
0 Min Read

Danny Jordaan ameshinda muhula wa nne kuongoza shirikisho la kandanda nchini Afrika Kusini  (SAFA) katika uchuguzi  ulioandaliwa Jumamosi.

Jordaan alipata kura 157  dhidi ya  82  za mpinzani wa  karibu Sandile Zungu.

Jordaan alipata ushindi kufuatia kuondolewa kwa maeneo 52 ya Zungu ambaye ni Mfyanyabiashara.

Jordan aliye na umri wa miaka 75 ameongoza SAFA tangu mwaka 2013.

Share This Article