Waaniaji tisa kutoka vyama tofauti wameidhinishwa na tume huru ya mipaka na Uchaguzi nchini (IEBC), kuwania ubunge wa Ol Kalou, katika uchaguzi unaotarajiwa kuandaliwa mwezi Julai.
Tisa hao ni; Abdulahi Abdifatah Hussein wa chama cha Federal Kenya,Timothy Kamau wa chama People’s Renaissance ,Samuel Muchina wa United Democratic Alliance, na Edward Mathenge, kutoka chama cha Kenya Moja Movement.
Wagombeaji wengine walioidhinishwa na IEBC ni ;Rachael Wangui wa chama cha People’s Democratic Party,Wilson Kigwa wa Jubilee,Stephen Wanyoike wa chama cha National Liberal,Kamau Ngotho wa Democray for Citizens na Ethe dwin Muchiri wa PNU.
Kiti hicho kilibaki wazi kufuatia kifo cha aliyekuwa Mbunge , David Kiaraho.
Uchaguzi huo mdogo utaandaliwa Julai 16 mwaka huu.