Duale ataka mageuzi yanayotekelezwa na KEMSA kuharakishwa

Tom Mathinji
1 Min Read
Waziri wa Afya Aden Duale ashauriana na bodi ya usimamizi ya KEMSA.

Waziri wa Afya Aden Duale, ameagiza Halmashauri ya Kusambaza Dawa Nchini KEMSA , kuharakisha utekelezaji wa marekebisho kuambatana na ajenda ya afya ya serikali chini ya mpango wa Botto Up, na kufanikisha  mpango wa Bima ya Afya kwa wote UHC.

Akiongea wakati wa mkutano wa mashauriano na bodi ya usimamizi ya KEMSA pamoja na maafisa wakuu wa halmashauri hiyo katika eneo la Embakasi, jijini Nairobi, Duale alisisitiza umuhimu wa kurejesha imani ya wananchi  kwenye shughuli ya  kusambaza dawa, ambayo huanza na mageuzi ya kitaasisi, ufanisi na uongozi wenye maadili.

Duale alipongeza mabadiliko yanayotekelezwa na KEMSA na kuitaka halmashauri hiyo kuharakisha  utekelezaji wa kanuni chini ya sheria  inayosimamia  halmashauri  ya KEMSA.

Duale aliitaka  KEMSA kudumisha umoja, uadilifu na uwajibikaji  ili kufanikisha mpango wa afya kwa wote.

Duale alikuwa ameandamana na Mkurugenzi Mkuu wa Afya Dkt. Patrick Amoth na viongozi wa KEMSA akiwemo Afisa Mkuu Mtendaji wa KEMSA Dkt. Ejersa Waqo.

Website |  + posts
Share This Article