Chui na Bandari washinda, Tusker, Police na Shabana wakabwa koo

Dismas Otuke
1 Min Read

Klabu ya AFC Leopards imesajili ushindi wa bao moja kwa bila dhidi ya Nairobi City Stars katika mojawapo wa mechi za Ligi Kuu FKF zilizosakatwa Jumapili.

Ingwe walipata bao pekee na la ushindio katika dakika ya 5 ya ngongeza kipindi cha pili kupitia kwa Kayci Odhiambo uwanjani Dandora, ukiwa ushindi wa nane msimu huu.

Kwenye matokeo mengine, wageni Bandari walisajili ushindi wa mbao 3-2 ugenini kwa Murang’a Seal, nao Police FC wakashikwa koo kwa kutoka sare ya bao moja na Sofapaka.

Shabana FC wakiwa nyumbani katika uchanjaa wa Gusii wametoka sare tasa na Kariobangi Sharks huku Tusker FC pia wakiumiza nyasi bila lengo maalum dhidi ya Kenya Commercial.

TAGGED:
Share This Article
Leave a Comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *