Chelsea wajaa fainali ya klabu bingwa Duniani

Joao Pedro alipachika mabao yote, moja katika kila kipindi, na kuwapa the Blues ushindi maridhawa.

Dismas Otuke
1 Min Read
EAST RUTHERFORD, NEW JERSEY - JULY 08: Joao Pedro of Chelsea FC scores his team's second goal whilst under pressure from Ignacio and Thiago Silva #3 of Fluminense FC during the FIFA Club World Cup 2025 semi-final match between Fluminense FC and Chelsea FC at MetLife Stadium on July 08, 2025 in East Rutherford, New Jersey. (Photo by Dan Mullan/Getty Images)

Klabu ya Chelsea ilijikatia tiketi kwa fainali ya klabu bingwa duniani baada ya kuwabandua Fluminense kutoka Brazil, mabao 2-0, kwenye nusu fainali iliyosakatwa jana Jumanne usiku katika uwanja wa Metlife mjini New Jersey.

Joao Pedro alipachika mabao yote, moja katika kila kipindi, na kuwapa The Blues ushindi maridhawa.

Nusu fainali ya pili itakasatwa leo usiku baina ya mabingwa wa Ulaya Paris St Germain, PSG kutoka Ufaransa dhidi ya Mabingwa mara 15 wa Ulaya Real Madrid.

Fainali ya kipute hicho itasakatwa Jumapili hii, Julai 13 katika uchanjaa wa Metlife.

Share This Article