Romania imemfukuza balozi wa Urusi kutoka nchini humo, na kufunga ubalozi wa Urusi, baada ya ndege mbili zisizo na rubani za Urusi kushambulia eneo la makazi nchini Romania.
Watu wawili wamejuruhiwa katika shambulio hilo mashariki mwa mji wa Galati.
Romania imemtaja balozi wa Urusi nchini humo kama “mtu asiyekubalika”
Msemaji wa rais wa Urusi amesema Vladimir Putin anafahamu kuhusu ajali ya ndege zisizo na rubani iliyotokea Romania.
Vyombo vya habari vya Urusi vimesema taifa hilo litajibu hatua ya Romania ya kumfukuza balozi wa taifa hilo kutoka nchini humo.
Watu wawili wamejeruhiwa baada ya ndege isiyo na rubani ya Urusi kugonga jengo la ghorofa katika mji wa Galati nchini Romania, karibu na mpaka wa Ukraine,hii ni kulingana na wizara ya ulinzi ya Romania.
Taarifa ya BBC.