Tuesday, 26 May 2026

Welcome to the official Kenya Broadcasting Corporation (KBC) News YouTube channel.

 
Explore Now
KBC Swahili
  • Habari
  • Biashara
  • Burudani
  • Michezo
  • Kimataifa
    • Habari Kuu
  • Back to KBC
  • Kimataifa
  • Habari Kuu
  • Michezo
  • Burudani
  • Biashara
  • Habari
  • Makala
KBC SwahiliKBC Swahili
Font ResizerAa
  • Habari
  • Biashara
  • Burudani
  • Michezo
  • Kimataifa
  • Back to KBC
Search
  • Habari
  • Biashara
  • Burudani
  • Michezo
  • Kimataifa
    • Habari Kuu
  • Back to KBC
Have an existing account? Sign In
Follow US
© 2022 Foxiz News Network. Ruby Design Company. All Rights Reserved.
Home Blog Baba Kaunty aondoka kwenye Obina Show
Burudani

Baba Kaunty aondoka kwenye Obina Show

Mchekeshaji huyo sasa anaangazia uundaji wa maudhui mitandaoni.

Marion Bosire
February 11, 2025 4:03 pm
By Marion Bosire
Share
2 Min Read
SHARE

Mchekeshaji kwa jina Baba Kaunty ambaye awali alifahamika kama Mama Kaunty, amesema kwamba ameodnoka kwenye kipindi cha mitandaoni cha Obina Show.

Baba Kaunty alichapisha video mitandaoni akielezea uamuzi wake wa kujiondoa kwenye kipindi hicho akisema haukuwa uamuzi rahisi.

Kwenye video hiyo, mchekeshaji huyo alisema alikuwa akiwaza kuhusu kuondoka kwa muda wa miezi kadhaa na akasisitiza kwamba hakushurutishwa na yeyote kuondoka.

Hata ingawa hakutaka kuzungumzia suala hilo hadharani, Baba Kaunty alisema alilazimika kupaaza sauti ili kuzuia minong’ono isiyo sahihi.

Migogoro kuhusu mipangilio katika kipindi cha Obina Live ni mojawapo ya sababu ambazo zilimfanya Baba Kaunty aondoke.

Anasema kipindi hicho hupeperushwa kila Jumatatu na kuna shughuli nyingine ambazo anapaswa kufanya Jumatatu kama vile mafunzo ambayo anasema yataendelea kwa miezi mitatu.

Mimi Mars aondoka hospitalini
Binti ya Angelina Jolie na Brad Pitt aanza mchakato wa kuondoa jina ‘Pitt’
Vivianne Ke asema familia yake ilimtesa alipokuwa akipitia talaka
Jaji aagiza kuharibiwa kwa stakabadhi zilizotwaliwa kutoka kwa seli ya Diddy

Jamaa huyo alimsifia Obina akimtaja kuwa mfano wa kuigwa na ndugu ambaye alimpa fursa ya kujifunza mengi akiongeza kwamba Obina pekee ndiye anaelewa maono yake.

Baba Kaunty sasa ataangazia uundaji wa maudhui ya mitandaoni pamoja na watoto wa mtaa wa mabanda wa Kibera kupitia kwa wakfu wake uitwao Baba Kaunty Initiative.

Nafasi yake katika kipindi cha Obina imechukuliwa na binti kwa jina Pamela ambapo Baba Kaunty anasema yeye ndiye alimpendekeza na kuwasiliana naye ili achukue nafasi hiyo.

Baba Kaunty ndiye wa pili kuondoka kwenye Obina Live Show baada ya Dem wa Facebook ambaye aliamua kutozungumzia suala hilo.

TAGGED:Baba KauntyDem wa FacebookObina Show LivePamela
Share This Article
Email Copy Link Print
Previous Article Serikali yawasihi wafanyabiashara kutoka Saudia kuwekeza Kenya
Next Article Uongozi wa KBC waifariji familia ya Mambo Mbotela

You May also Like

Burudani

Masaka Kids kuangaziwa kwenye Netflix

September 16, 2025
Burudani

Nazizi amkumbuka mwanawe aliyefariki

September 27, 2025
Burudani

Davido kuchangia mayatima kwenye siku yake ya kuzaliwa

November 18, 2024
Burudani

Mali Safi Chito asema amerejea nyumbani

September 10, 2025
Show More
  • More News:
  • Kenya
  • William Ruto
  • CAF
  • Tanzania
  • President William Ruto
  • Uganda
  • DCI
  • FKF
  • Rais William Ruto
  • Israel
  • USA
  • Nigeria
  • Raila Odinga
  • FIFA
  • Musalia Mudavadi
  • EACC
  • Rigathi Gachagua
  • DRC
  • IEBC
  • ODM
KBC Swahili

Information You Can Trust: Stay instantly connected with breaking stories and live updates. From politics and technology to entertainment and beyond, we provide real-time coverage you can rely on, making us your dependable source for 24/7 news.

Youtube Medium Rss

About Company

  • Contact Us
  • Advertise with US
  • Complaint
  • Privacy Policy
  • Cookie Policy
  • Submit a Tip

Real-time Updates on the Latest Stories!

© Kbc Swahili.  All Rights Reserved. 2025

Welcome to Foxiz
Username or Email Address
Password

Lost your password?