Mashindano ya kuwania Kombe la mataifa ya Afrika (AFCON), kwa chipukizi chini ya umri wa miaka 17, yanayoendelea nchini Morocco, ni dhihirisho la hatua mwafaka, zilizochukuliwa na Serikali ya Kifalme nchini Morocco, katika ukuzaji vipaji.
Taifa hilo la Kaskazini mwa Afrika kupitia kwa Ajenda ya mwaka 2009, ya Mfalme Mohammed wa sita wa Morooco, ya kuweka taifa hilo kuwa kielelezo barani Afrika.
Ujumuishwaji kwa wachezaji wanne wanaotokea katika Akademia ya Mohammed 6, soka ya chipukizi ikiwa mojawapo wa ruwaza ya muda mrefu ya makuzi ya vipaji vya soka.
Akademia ya Mohammed 6 ilizinduliwa mwaka 2009, ili kuleta utaalam na ufundi wa soka kupitia kwa kuwepo wa miundombinu ya kisasa.

Leo hii ukitembea Morocco kufuatilia AFCON kwa chipukizi ya umri wa miaka 17,utapata wachezaji wapya kama vile Ibn Salah Oualid, Boughazir Adam, Harouch Mohamed, na Ezzarky Ayman, ni baadhji ya wachezaji walitokea kaika mifumo ya chipukizi.
Wanandinga hao wanafuata nyayo za wachezaji nyota katika fainali za Kombe la Dunia mwaka 2022, kama vile Youssef En-Nesyri, Nayef Aguerd,na Azzedine Ounahi.