AFCON U20 kuingia hatua ya nane bora kesho nchini Misri

Timu zitakazofuzu kwa nusu fainali zitawakilisha Afrika kwenye fainali za Kombe la dunia nchini Chile kati ya Septemba na Oktoba mwaka huu.

Dismas Otuke
1 Min Read

Kipute cha kuwania kombe la mataifa ya Afrika kwa chipukizi chini ya umri wa miaka 20, kitaingia hatua ya robo fainali kesho nchini Misri.

Mabingwa mara saba Nigeria watakumbana na mabingwa watetezi Senegal kuanzia saa tisa, kabla ya wenyeji kupimana nguvu na Ghana saa kumi na mbili huku Morocco wakiwa na miadi dhidi ya Sierra Leone.

Afrika Kusini watamaliza udhia na Jamhuri ya Demokrasia ya Congo saa tatu usiku.

Timu zitakazofuzu kwa nusu fainali zitawakilisha Afrika kwenye fainali za Kombe la dunia nchini Chile kati ya Septemba na Oktoba mwaka huu.

Website |  + posts
TAGGED:
Share This Article