Timu za uokoaji nchini Nepal zimo mbioni kutafuta manusura zaidi wa mafuriko makubwa ya ghafla yaliyotokea nchini humo Agosti 26 mwaka huu.
Mafuriko hayo yalitokea kwenye eneo la mpaka na China.
Timu hizo zimeimarisha jitihada za kuwatafuta wafanyakazi watu waliokwama ndani ya mitambo ya umeme huku ripoti zikiashiria yamkini baadhi yao bado wako hai.
Mamlaka nchini Nepal zinasema watu 1,259 wamefariki tangu kutokea kwa mkasa huo huku wengine zaidi ya 5,000 wakiwa hawajulikani walipo.
Ripoti za vyombo vya habari nchini China zinaashiria watu 21 wamefariki kutokana na janga hilo nchini humo huku wengine zaidi ya 540 wakiwa hawajulikani walipo.
Ripoti zinaashiria takriban watu 900 wamekwama katika mitambo mbalimbali ya umeme.