Tusker FC waelekea Rwanda kukabiliana na Al Ahli Madani,Kombe la Shirikisho

Wagema Mvinyo Tusker wanarejea kwenye kipute hicho kwa mara ya kwanza baada y kuwa nje kwa miaka minne ,mara ya mwisho wakishiriki ikiwa msimu wa mwaka 2021/2022.

Dismas Otuke
1 Min Read

Tusker FC wameondoka nchini Jumatano jioni keulekea Kigali,Rwanda, kwa mkumbo wa kwanza wa mchujo wa kwanza kuwania kombe la Shirikisho dhidi ya Al Ahli Madani .

Tusker watakabiliana na Al Ahli Madani Jumamosi hii Septemba 5, huku marudio yakipigwa Septemba 12 jijini Nairobi.

Wagema Mvinyo Tusker wanarejea kwenye kipute hicho kwa mara ya kwanza baada y kuwa nje kwa miaka minne ,mara ya mwisho wakishiriki ikiwa msimu wa mwaka 2021/2022.

Aidha,Tusker wanajivunia kucheza hadi fainali ya Kombe hilo mwaka 1994.

Tusker walifuzu kuiwakilisha Kenya baada ya kunyakua Kombe la Mozzart Bet.

Share This Article