Iran yadai kuidungua ndege isiyo na rubani ya Marekani

radiotaifa
1 Min Read
Picha kwa hisani ya EPA

Iran imesema imeidungua na kuharibu ndege isiyo na rubani ya Marekani aina ya MQ 9, ambayo inadai ilikuwa ikiruka juu ya mji wa Andimeshk.

Kwa mujibu wa Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC), ndege hiyo ilidunguliwa kwa kutumia mfumo wa kisasa wa ulinzi wa anga.

Shirika la habari la Tasnim, linalohusishwa na IRGC, liliripoti kuwa operesheni hiyo ilifanikiwa, lakini halikutoa ushahidi wa kuthibitisha madai hayo.

Hadi sasa, Marekani wala Kamandi Kuu ya Jeshi la Marekani (CENTCOM) hawajathibitisha rasmi madai ya Iran kwamba ndege hiyo ya MQ 9 ilidunguliwa.

Taarifa ya BBC

TAGGED:
Share This Article