Taarifa ya BBC:
Vikosi vya Ukraine vimeshambulia mojawapo ya “viwanda muhimu vya kijeshi” vya Urusi, Rais Volodymyr Zelensky amesema.
“Kiwanda hicho kinazalisha vifaa vya elektroniki na vifaa vya makombora ya Urusi. Makombora yenyewe hutumika kushambulia miji yetu, vijiji vyetu na raia,” alisema.
Makombora ya British Storm Shadow yalitumiwa kushambulia kiwanda cha Kremniy El katika eneo la mpaka la Bryansk, jeshi la Ukraine lilisema.
Mamlaka za mitaa za Urusi zimesema takriban raia sita waliuawa na 42 kujeruhiwa katika “shambulio la kombora la kigaidi”.
Msemaji wa Rais Vladimir Putin alisema ni “dhahiri kwamba urushaji wa makombora haya hauwezekani bila wataalamu wa Uingereza”.