Thursday, 16 Jul 2026

Welcome to the official Kenya Broadcasting Corporation (KBC) News YouTube channel.

 
Explore Now
KBC Swahili
  • Habari
  • Biashara
  • Burudani
  • Michezo
  • Kimataifa
    • Habari Kuu
  • Back to KBC
  • Kimataifa
  • Habari Kuu
  • Michezo
  • Burudani
  • Biashara
  • Habari
  • FIFA WORLD CUP 2026
  • Makala
KBC SwahiliKBC Swahili
Font ResizerAa
  • Habari
  • Biashara
  • Burudani
  • Michezo
  • Kimataifa
  • Back to KBC
Search
  • Habari
  • Biashara
  • Burudani
  • Michezo
  • Kimataifa
    • Habari Kuu
  • Back to KBC
Have an existing account? Sign In
Follow US
© 2022 Foxiz News Network. Ruby Design Company. All Rights Reserved.
Home Blog Dem wa Facebook aghadhabishwa na wasanii wa kwao Kitale
Burudani

Dem wa Facebook aghadhabishwa na wasanii wa kwao Kitale

Marion Bosire
September 8, 2024 8:21 am
By Marion Bosire
Share
1 Min Read
SHARE

Mwanamitandao Milicent Aywa almaarufu Dem wa facebook alionekana kupandwa na mori kutokana na vitendo vya wasanii wa nyumbani kwao Kitale.

Wasanii hao ambao awali walianzisha kampeni mitandaoni ya kukana hafla alizokuwa amepanga Milicent walimfumania Obinna ambaye hufanya kazi na Dem wa Facebook wakitaka kujumuishwa kwenye onyesho hilo.

Video iliyosambazwa mitandaoni ilionyesha wasanii hao wakiwa wamezingira gari ya Obinna wakitaka kuzungumza naye huku wakilalamika kwamba aliwarejelea kama wasanii wa mtaani.

Kulingana na Obinna mmoja wa wasanii hao alimtukana akitafuta kile alichokitaja kuwa “haki yake” ya kujumuishwa kwenye tamasha na baadaye alipwe.

Msanii huyo alionekana kughadhabishwa na usemi wa Obinna akisema yeye sio msanii wa mtaani, alipoulizwa iwapo yeye ni wa kimataifa akaonekana kuchanganyikiwa.

Katika kikao na wasanii hao, Millicent aliwakosoa akisema wamekasirisha mkubwa wake kikazi ambaye amempa fursa ya kukua katika fani yake na ndio mara ya kwanza amempeleka nyumbani.

Mwanamuziki wa Tanzania Haitham Kim aaga dunia
Cardi B afika mahakamani kujitetea katika kesi ya dhuluma
Mwanamitandao Tabitha Gatwiri afariki
Cindy Sanyu apendekeza shindano la Ava Peace na Jowy Landa

“Hayo matusi mmetusi Obinna mngeniwekea mimi. Mimi ndio msichana wenu wa nyumbani, sio Obinna. Obinna ni mkubwa wangu.” alisema Dem wa Facebook.

Inaaminika kwamba waliafikiana kwani usiku wa jana video ilisambazwa ikionyesha wasanii hao jukwaani ila umati uliokuwepo haukuridhishwa na tumbuizo lao.

TAGGED:Dem wa FacebookHomecomingKitaleOga Obinna
Share This Article
Email Copy Link Print
Previous Article Moto wazuka katika shule ya upili ya wasichana ya Isiolo
Next Article Chameleone asema hadithi ya wimbo Jamila ni ya ukweli

You May also Like

Burudani

Titi Brown aanzisha mpango wa kutangaza utalii wa Rwanda

July 1, 2026
Burudani

Bien na Diamond watoa kibao cha pamoja – Katam

June 9, 2025
Burudani

Multichoice yawarai Wakenya kuunga mkono sinema za humu nchini

April 8, 2024
Burudani

Mwijaku ammiminia mkewe sifa kama njia ya kuzima uvumi kumhusu

April 21, 2025
Show More
  • More News:
  • Kenya
  • William Ruto
  • CAF
  • Tanzania
  • President William Ruto
  • Uganda
  • FIFA
  • DCI
  • FKF
  • Rais William Ruto
  • USA
  • Israel
  • Nigeria
  • DRC
  • Raila Odinga
  • Musalia Mudavadi
  • EACC
  • Rigathi Gachagua
  • Morocco
  • IEBC
KBC Swahili

Information You Can Trust: Stay instantly connected with breaking stories and live updates. From politics and technology to entertainment and beyond, we provide real-time coverage you can rely on, making us your dependable source for 24/7 news.

Youtube Medium Rss

About Company

  • Contact Us
  • Advertise with US
  • Complaint
  • Privacy Policy
  • Cookie Policy
  • Submit a Tip

Real-time Updates on the Latest Stories!

© Kbc Swahili.  All Rights Reserved. 2025

Welcome to Foxiz
Username or Email Address
Password

Lost your password?