Washirika wa Ukraine kuondoa mafuta na gesi ya Urusi kwenye soko la kimataifa

Tom Mathinji and BBC
1 Min Read

Zaidi ya mataifa 20 yanayoiunga mkono Ukraine yameahidi “kuondoa mafuta na gesi ya Urusi katika soko la kimataifa” kama sehemu ya juhudi za kumshinikiza Rais Vladimir Putin kukomesha vita.

“Tunazuia ufadhili wa nguvu ya kijeshi ya Urusi,” alisema Waziri Mkuu wa Uingereza Sir Keir Starmer, baada ya kuandaa mkutano wa kilele wa “muungano wa walio tayari” jijini London.

Uingereza na Marekani katika siku za hivi karibuni zimeweka vikwazo dhidi ya makampuni mawili makubwa ya mafuta ya Urusi, huku EU ikilenga mauzo ya nje ya gesi asilia iliyoyeyushwa (LNG) ya Moscow.

Rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky, ambaye pia alikuwa London, alisema “shinikizo” kwa Urusi ndiyo njia pekee ya kusimamisha mapigano.

Hata hivyo, hakuna uwasilishaji wa makombora ya masafa marefu kwenda Ukraine uliotangazwa katika mkutano huo.

Website |  + posts
TAGGED:
Share This Article