Uwanja wa michezo wa Talanta unaojengwa katika barabara ya Ngong pamoja na uwanja wa ndege wa Kisumu, zitabadilishwa jina na kuitwa Raila Odinga stadium na Raila Odinga International Airport mtawalia.
Haya yametangazwa na Rais William Ruto katika mahojiano ya moja kwa moja na Wanahabari wa eneo la Luo Nyanza Jumatatu jioni.
Ruto alisema hatua hiyo inalenga kutoa heshima kwa Waziri Mkuu wa zamani aliyefariki mwaka uliopita, hayati Raila Odinga.
Uwanja wa Talanta unaomudu mashabiki 60,000, utakuwa mojawapo wa viwanja viwili vikuu nchini nchini vitakavyotumika kuandaa fainali za kombe la AFCON mwaka 2027.