Upasuaji wa Ojwang kufanyika leo

Hatua hiyo ililazimu wapasuaji wa serikali kuahirisha shughuli hiyo hadi leo Jumanne.

Dismas Otuke
1 Min Read

Upasuaji wa Mwanablogu  na Mwalimu Albert Omondi Ojwang, utafanyika  leo kubaini chanzo cha kifo chake mikononi mwa  polisi.

Usalama uliimarishwa nje na ndani ya makafani ya City mapema Jumanne,baada ya makundi ya wanaharakati wakiandamana na familia  kuvuruga shughuli walipozingira eneo ambalo mwili huo umehifadhiwa Jumatatu .

Hatua hiyo ililazimu wapasuaji wa serikali kuahirisha shughuli hiyo hadi leo Jumanne.

Polisi walisema kuwa marehemu Ojwang alipatikana akiwa amepoteza fahamau katika  kororkoro ya kituo cha Central, wakisema kuwa huenda lilikuwa jaribio la kujiua.

Ojwang pamoja na  mshatikiwa mwingine Kelvin Moinde, walikabiliwa na kesi ya kuchapisha habari za uongo kumhusu Naibu Kamishnaa Mkuu wa Polisi Eliud Lagat.

Website |  + posts
Share This Article