Shirika la reli nchini lilisafirisha mizigo kutoka kituo cha Athi River,kupitia Gilgil-Nyahururu, kwa mara ya kwanza,ikiwa miaka 46, tangu treni hiyo ya mizigo kusitishwa.
Katika safari hiyo ya kwanza treni ilisafirisha tani 396 za mbolea ya serikali iliyopunguzwa bei kutoka kwa ghala la halmashauri ya nafaka na mazao (NCPB ),katika kituo cha Athi River hadi Nyahururu.
Mbolea hiyo itratumika na Wakulima wa Nyahururu na Laikipia.
Treni hiyo inatarajiwa kufungua fursa nyingi za kibiashara kati ya Nyahuru na Athi River.
Aidha, usafiri wa treni kati ya Athi River na Nyahururu utapunguza gaharama ya usafiri.