Dkt.Patrice Motsepe, amechaguliwa bila kupingwa kwa muhula wa pili kuwa Rais wa Shirikisho la kandanda barani Afrika (CAF).
Motsepe amechaguliwa kwenye kikao kisicho cha kawaida, kilichoandaliwa leo jijini Cairo Misri.
Kinara huyo atasalia afisini kwa kipindi kingine cha miaka minne.
Kikao hicho kimehudhuriwa na Rais wa FIFA Gianni Infantino.