Iran yasema inapendelea mazungumzo, lakini iko tayari kwa vita pia

radiotaifa
1 Min Read
Picha kwa hisani ya CBS

Mazungumzo ya kidiplomasia kati ya Iran na Marekani yanaendelea huku Iran ikisisitiza kuwa, pamoja na kuipa kipaumbele njia ya mazungumzo, bado iko tayari kurejea vitani ikiwa juhudi hizo zitashindwa.

Hayo yameelezwa na mpatanishi mkuu wa upande wa Iran, Mohammad Bagher Ghalibaf, ambaye alisema katika mahojiano na televisheni ya taifa kuwa Tehran haitaacha kujilinda iwapo mazungumzo hayatatoa matokeo.

“Tunafuata njia ya mazungumzo, lakini ikiwa mazungumzo hayatatekelezwa, pia tuko tayari kwa vita na tutajibu ipasavyo,” alisema Ghalibaf.

Kauli hiyo ilitolewa wakati wajumbe wa Iran na Marekani walipokuwa wakitarajiwa kufanya mazungumzo mengine mjini Doha, yakilenga kupunguza mvutano na kutafuta suluhu ya kudumu ya mgogoro uliodumu kwa miezi kadhaa.

Mvutano huo uliongezeka mwezi Juni 2026, baada ya mashambulizi ya kijeshi kati ya Iran na Israel, yaliyohusisha pia mashambulizi ya Marekani dhidi ya baadhi ya maeneo ya nyuklia ya Iran. Baada ya siku kadhaa za mapigano, pande husika zilikubaliana kusitisha mapigano kwa muda ili kutoa nafasi kwa juhudi za kidiplomasia.

Ingawa mapigano yamesitishwa kwa sasa, bado hakuna makubaliano ya kudumu yaliyofikiwa.

Taarifa ya BBC

Share This Article