Huduma za Intaneti kurejeshwa nchini Iran

KBC Digital News
1 Min Read
Huduma za intaneti zarejeshwa nchini Iran.

Rais wa Iran, Masoud Pezeshkian, ameagiza Wizara ya Mawasiliano kurejesha huduma za intaneti nchini katika hali iliyokuwapo kabla ya Desemba 2025.

Naibu Waziri wa Mawasiliano amethibitisha kupokea agizo hilo, akisema kuwa hatua hiyo ni sehemu ya juhudi za kurejesha haki za wananchi na kuimarisha imani ya umma kwa serikali.

Vyombo vya habari vya serikali ya Iran vimeripoti kuwa katika kikao kilichoongozwa na Makamu wa Rais, Mohammad Reza Aref, maamuzi muhimu kuhusu hali ya intaneti nchini yaliidhinishwa.

Taarifa hiyo ilieleza kuwa baada ya idhini ya mwisho kutoka kwa Rais Pezeshkian, maagizo rasmi yatatolewa kwa Wizara ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari ili kuyatekeleza.

Kwa mujibu wa shirika la habari la Fars, pendekezo la kurejesha huduma za intaneti liliidhinishwa kwa kura tisa za kuunga mkono na baadaye kuwasilishwa katika ofisi ya rais kwa ajili ya idhini ya mwisho.

Huduma za intaneti nchini Iran zilisitishwa wakati wa operesheni za kukabiliana na maandamano yaliyotokea Desemba mwaka jana.

Baadaye, zilipunguzwa tena kufuatia mashambulizi yaliyotekelezwa na Israel na Marekani dhidi ya Iran. Hatua ya sasa inaashiria uwezekano wa kurejea kwa huduma za mawasiliano kwa kiwango kikubwa baada ya miezi kadhaa ya vikwazo.

Taarifa ya BBC.

TAGGED:
Share This Article