Ambani ndiye Mwenyekiti mpya wa AFC Leopards

Mshambulizi huyo wa zamani wa Kenya na pia mchezaji wa zamani wa Leopards amezoa kura  1,101  dhidi ya mpinzani wake  Vincent Enos Mutoka aliyepata kura 682.

Dismas Otuke
1 Min Read

Boniface Ambani amechaguliwa Mwenyekiti mpya wa klabu ya  AFC Leopards, baada ya kubuka mshindi wa uchaguzi wa Jumapili.

Mshambulizi huyo wa zamani wa Kenya na pia mchezaji wa zamani wa Leopards amezoa kura  1,101  dhidi ya mpinzani wake  Vincent Enos Mutoka aliyepata kura 682.

Isaac Mulindi ndiye Katibu Mkuu kwa kupata kura  678 akifuatwa na Robert Situma aliyepata kura  534,huku Irene Sitawa akichukua nafasi ya tatu kwa kura 529 .

Newton Lime Luchacha amechaguliwa mweka hazina kwa kupata kura 676,akiwashinda Edwin Chamwada na Patrick Kanyangi waliopata kura 599 na 445 mtawalia.

Ambani anatwaa Uenyekiti  kutoka kwa Dan Shikanda, ambaye amehudumu kwa mihula miwili.

 

Website |  + posts
Share This Article