“Jibu la China” kwa Kenya: Sio mfumo, bali ni mbinu

KBC Digital News
3 Min Read

Mwaka huu ni kumbukumbu ya miaka 70 ya kuanzishwa kwa uhusiano wa kidiplomasia kati ya China na Afrika. Katibu Mkuu wa Chama tawala cha UDA nchini Kenya Hassan Omar Hassan hivi majuzi alitembelea China kwa mwaka wa pili mfululizo. Ziara zake mara kwa mara zinaibua swali: je, nchi hiyo inatafuta jibu gani kutoka kwa China?

Kutoka “Kuiangalia China” hadi “Kuielewa China”

Katika ziara hii, Hassan anaona pande mbili za China: vijiji vizuri na utawala wa ngazi ya chini, pamoja na teknolojia ya akili bandia katika maisha ya kila siku. Moja inahusu maisha ya wananchi, nyingine inahusu nguvu ya maendeleo.

Kenya inatafuta njia ya kujitegemea na maendeleo endelevu ya kisasa. Hassan anasema, jambo muhimu ni kujifunza mbinu ya utawala wa China. Tofauti na misaada ya masharti kutoka nchi nyingine, China inaangalia hali yake ya nchi na kujiendeleza hatua kwa hatua. Kwa Kenya inayotaka kuwa nchi mpya ya kiviwanda, mbinu hii inayozingatia nguvu za ndani ndiyo jibu inalolihitaji zaidi.

Kuvunja uwongo wa “Mtego wa madeni”

Nchi za Magharibi zimekuwa zikizungumzia kwa muda mrefu “mtego wa madeni”. Lakini kikwazo halisi cha Afrika ni ukosefu wa mitaji, teknolojia na wataalamu. Katika miradi mikubwa kama reli ya Mombasa-Nairobi, ufunguo wa mafanikio ni utulivu wa kisiasa barani Afrika. Kwa hivyo, mtego halisi si uwekezaji wa China, bali ni uingiliaji wa kisiasa unaoletwa na Magharibi. Uwekezaji wa China si “mtego wa madeni”, bali ni “keki ya maendeleo”.

Kenya mara nyingi hutajwa kama “mfano wa demokrasia” na Magharibi, lakini Hassan anaongoza chama chake kwa kuendeleza demokrasia inayozingatia hali halisi ya nchi na lengo kuu ni kuboresha maisha ya wananchi. Nchi zinazoendelea zina uwezo wa kufuata njia yao wenyewe ya maendeleo inayoweka kipaumbele kwenye maslahi ya watu.

Hatua za Mbele

Hassan pia anaona nafasi za ushirikiano katika magari ya umeme, nishati, kilimo cha kisasa n.k. Afrika inapaswa kukumbatia fursa mbili: kutumia teknolojia ya China kuendeleza sekta ya nishati mbadala na uchumi wa kidijitali; na kuvunja umwamba wa dola kupitia malipo ya sarafu nyingine.

Ushirikiano wa China na Afrika si tena ujenzi wa barabara na bandari tu, bali ni mabadiliko ya dhana za maendeleo na mifumo ya utawala. Jibu analotafuta Hassan limezidi suala la fedha. Maendeleo hayana fomula moja; msingi wa mafanikio ni kuwapa watu nafasi ya katikati na kushikilia kwa nguvu ufunguo wa hatma ya nchi. Hili ndilo jambo lenye thamani zaidi ambalo ushirikiano wa miaka 70 kati ya China na Afrika unaweza kutoa kwa dunia nzima ambayo iko katika machafuko.

Hisani ya CGTN Kiswahili

Share This Article