Mchezaji nyota wa Argentina Lionel Messi amekutana na Rais wa Marekani Donald Trump, kwa mara ya kwanza katika Ikulu ya White House Alhamisi usiku.
Messi aliwaongoza wachezaji wa timu yake ya Inter Miami katika mwaliko huo wa Ikulu baada ya klabu hiyo kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu ya MLS mwaka 2025.