Shujaa kuchuana na Ireland kuwania nafasi ya 11 Vancouver

Dismas Otuke
1 Min Read

Timu ya taifa ya raga ya Kenya kwa wachezaji saba kila upande itachuana na Ireland leo usiku. Mechi hiyo itakuwa ya kuwania nafasi ya 11 na 12 katika msururu wa nne wa mashindano ya dunia ya Vancouver nchini Canada.

Kenya imepoteza mechi zote nne ilizocheza huko Vancouver.

Shujaa ilishindwa mechi tatu za kundi A dhidi ya Uingereza, Ufaransa na Argentina, kabla ya kulemewa na Uruguay katika mechi ya kuwania nafasi za 9 na 10.

Share This Article
Leave a Comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *