Ndege ndogo yaanguka Malindi, watu kadhaa wahofiwa kufariki

Mamlaka bado hazijathibitisha ajali hiyo ambayo chanzo chake bado hakijulikani.

Martin Mwanje
0 Min Read

Watu kadhaa wamehofiwa kufariki baada ya ndege ndogo kuripotiwa kuanguka na kuwaka moto katika eneo la Kowachocha huko Malindi, kaunti ya Kilifi. 

Yamkini watu wengine kadhaa wamejeruhiwa kutokana na ajali hiyo.

Chanzo cha ajali hiyo bado hakijajulikana.

Polisi wamefika eneo hilo wakati shughuli za uokozi zikiendelea.

Hata hivyo, mamlaka husika hazijathibitisha kutokea kwa ajali hiyo.

Tutakuletea taarifa za kina punde tukizipokea 

TAGGED:
Share This Article
Leave a Comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *